DOM LAND BLOG

DOM LAND BLOG

Tuesday, December 23, 2014

RC DAR APETA UJENZI WA MAABARA: AMPA RAIS JAKAYA KIKWETE ZAWADI YA MAFANIKIO

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Said Meck Sadick, akimkaribisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete kuzungumza na Wazee wa mkoa wa Dar es Salaam kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee ambapo alimpa taarifa Mheshimiwa Rais juu ya mafanikio ya ujenzi wa maabara katika Shule za Sekondari jijini Dar es Salaam kwa asilimia 100 pamoja na matokeo ya uchaguzi wa Serikali za Mitaa mkoa wa Dar es salaam kwa asilimia 76 ukiacha mitaa miwili ambayo uchaguzi haukufanyika kwa sababu ya vurugu ambapo wahusika wote wanashughulikiwa kisheria kutokana na vurugu walizosababisha.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akiwasalimia Wazee wa mkoa wa Dar es Salaam ambao waliitika wito wa kumsikiliza wakati wa kulihutubia Taifa kupitia Wazee kwenye Ukumbi wa Diamond Jubilee, jijini Dar es Salaam.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisoma hotuba yake kwa Wazee wa Mkoa wa Dar es Salaam kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es Salaam jana.
 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akihutubia Taifa kupitia Wazee wa Mkoa wa Dar es Salaam katika ukumbi wa Diamond Jubilee ambapo alizungumzia uchaguzi na kutaka polisi kufanya kazi yao katika kuhakikisha uchaguzi ujao  hauvurugwi na pia alifafanua mambo mbali mbali yaliyokuwa yakizungumziwa kuhusu akaunti ya Tegeta ESCROW na kumwajibisha Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Profesa Anna Tibaijuka.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akipanga vyema karatasi zenye hotuba yake wakati akiwahutubia Wazee wa mkoa wa Dar es Salaam jana.
 Ukumbi wa Diamond Jubilee ukiwa umefurika Wazee waliokuja kumsikiliza Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete.
 Baadhi ya Wanasiasa wakongwe waliohudhuria.
Rais Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na Mbunge wa Kinondoni Iddi Azzan muda mfupi baada ya kulihutubia taifa kupitia wazee wa Dar es Salaam jana kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es Salaam.
Rais Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akiwapungia mkono wananchi wakati akiwaaga jana mara baada ya kuzungumza na taifa kupitia wazee wa Dar es Salaam (picha na Freddy Maro).

No comments:

Post a Comment