Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana na
msafara wake ukiwa umezingirwa na wananchi wa jamii ya kimasai
ulipokuwa ukiondoka baada ya kuhutubia mkutano katika Kijiji cha
Mtakuja, Kata ya Kia, Jimbo la Hai, mkoani Kilimanjaro jana, wakati wa
ziara ya kuimarisha uhai wa chama, kukagua miradi inayotekelezwa kwa
kufuata Ilani ya Uchaguzi ya CCM, pamoja na kusikiliza kero za Wananchi
na kuzitafutia ufumbuzi.
Komredi Kinana ambaye katika ziara yake ameambatana na Katibu wa
Itikadiu na Uenezi, Nape Nnauye, ameutaka uongozi wa Kampuni ya Uwanja
wa Ndege wa Kilimanjaro kuacha kuwabughudhi wananchi wa kata hiyo, baada
ya kutoa mallamiko kuwa unataka kuwapora ardhi iliyo karibu na uwanja
huo yenye ukubwa wa zaidi ya hekali 10,000 inayomilikiwa na vijiji 11.
Komredi Kinana amekemea tabia hiyo ya baadhi ya viongozi wanaopora
kinguvu ardhi za wananchi. Pia amewahakikishia wananchi hao kuwa
atasaidia kurejesha ardhi hiyo kwa kukutana na Rais Jakaya Kikwete na
kumwambia juu ya dhulma hiyo.
Komredi Kinana , amesema kuwa kiongozi yeyote aliyeingia CCM kwa
minajiri ya kutaka kujineneemesha binafsi kimaisha, kwanzia sasa
hatakuwa na nafasi na inabidi aondoke katika chama hicho ambacho kazi
yake ni kutetea haki za wanyonge. |
No comments:
Post a Comment